Elimu ya Usuluhishi wa Migogoro ya Bima katika Maadhimisho ya Wiki ya Usafiri Endelevu Aridhini
27 Nov, 2025
Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima Tanzania (TIO) imeendelea kutoa elimu ya usuluhiushi wa migogoro ya bima kwa wananchi mbalimbali wanaotembelea banda katika maadhimisho ya Wiki ya Usafiri Endelevu Aridhini yaliyoandaliwa na LATRA.
Maadhimisho hayo yaliyoanza tarehe 24 Novemba na yanatarajiwa kumalizika Novemba 29, 2025 yamekuwa jukwaa muhimu kwa umma kufahamu shughuli mbalimbali zinazofanywa na ofisi hiyo na kupokea maoni mbalimbali.
Pichani ni Bi. Gloria Sindano Afisa Bima Mwandamizi kutoka TIO akitoa elimu ya Bima kwa wananchuo wa chuo cha Bandari waliotembelea banda.
