TIO tunashiriki maadhimisho ya Wiki ya Usafiri Endelevu aridhini
25 Nov, 2025
Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima inashiriki katika maadhimisho maalumu ya Wiki ya Usafiri endelevu aridhini yaliyoandaliwa na LATRA yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kuanzia Novemba 24 - 29, 2025.
TIO inaungana na taasisi mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu ya usuluhishi wa Migogoro ya bima kwa wananchi ambapo wananchi mbalimbali wametembelea banda kujifunza zaidi.
Wananchi wote mnakaribishwa katika banda letu kwa ajili kujifunza masuala mbalimbali ya usuluhishi wa Migogoro ya bima.
